Kulipokuwa asubui, yeye akiwa na wasiwasi sana, aliwaita wachawi wote wa Misri, na wenye hekima, akawaambia ndoto zake. Lakini hakuna hata mumoja aliyeweza kumutafsiria ndoto zile.
Kisha, kiumbe kimoja chenye umbo la mutu, kiliigusa midomo yangu, nami nilifungua midomo yangu na kumwambia huyo aliyesimama karibu nami: Ee bwana, maono haya yameniletea maumivu makali hata nimeishiwa nguvu.
Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:
Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Belsasari wa Babeli, Danieli aliota ndoto na kuona maono akiwa amelala katika kitanda chake. Akaandika ndoto yake hii:
Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Mawazo yangu yaliniogopesha sana mimi Danieli, hata rangi yangu ikabadilika. Lakini nilichunga jambo hilo ndani ya moyo wangu.
Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.