Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 7:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Belsasari wa Babeli, Danieli aliota ndoto na kuona maono akiwa amelala katika kitanda chake. Akaandika ndoto yake hii:

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 7:1
34 Iomraidhean Croise  

Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


Ilikuwa usiku wakati watu wanapoota ndoto, wakati usingizi muzito unawashika watu.


Mungu aliniambia: Sasa andika jambo hili mbele yao, juu ya kibao na katika kitabu, likuwe ushuhuda wa milele:


Yawe aliniambia hivi: Twaa ubao mukubwa, uandike juu yake maneno yanayosomeka waziwazi: “Teka haraka. Nyanganya Upesi.”


Nabii aliyeota ndoto, atangaze ndoto yake, lakini yule aliyefunuliwa ujumbe wangu autangaze kwa uaminifu. Kuna ulinganifu gani kati ya maganda na ngano? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mataifa yote yatamutumikia yeye, pamoja na mwana wake na mujukuu wake mpaka wakati inchi yake itakapoanguka. Kisha mataifa mengi na wafalme wengi wakubwa watamufanya kuwa mutumwa wao.


Kisha, Yeremia alitwaa kitabu kingine, akamupa katibu Baruku mwana wa Neria, ambaye aliandika humo maneno yote aliyoambiwa na Yeremia ambayo yalikuwa katika kile kitabu cha mbele ambacho Yoyakimu, mufalme wa Yuda, alichoma kwa moto. Maneno mengine ya namna hiyo yaliongezwa.


Halafu Yeremia akamwita Baruku mwana wa Neria. Naye Baruku akaandika katika kitabu maneno yote yaliyotoka katika kinywa cha Yeremia sawa vile Yawe alivyokuwa amemwambia.


Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.


Basi, nikiwa katika maono Yawe akanipeleka mpaka katika inchi ya Israeli, akaniweka juu ya mulima murefu sana, na upande wa kusini kulikuwa majengo yaliyoonekana kama muji.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Katika mwaka wa pili wa utawala wake, mufalme Nebukadneza aliota ndoto. Na kwa hiyo roho yake ikahuzunika sana hata hakuweza kupata usingizi.


Mufalme akamwuliza Danieli, ambaye vilevile aliitwa Beltesaza: Unaweza kunijulisha ndoto niliyoota na maana yake?


Akili yake ya kimutu ibadilishwe, akuwe na akili ya nyama kwa miaka saba.


Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:


Siku moja mufalme Belsasari alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakubwa wake na kunywa divai pamoja nao.


Lakini wewe Belsasari mwana wake, ingawa unayajua haya yote, haukujinyenyekeza!


Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.


Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake.


Maono niliyoyaona mimi Danieli yaliniogopesha, nami nikafazaika.


Kisha, katika maono hayo yangu ya usiku, nikaona nyama wa ine wa ajabu na wa kutisha, mwenye nguvu sana. Huyu alikuwa na meno makubwa ya chuma ambayo aliyatumia kwa kula na kuvunjavunja, na mabaki aliyakanyagakanyaga. Alikuwa tofauti na wale nyama wengine watatu, maana alikuwa na pembe kumi.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Belsasari, mimi Danieli nikapata maono mengine zaidi ya maono yale ya kwanza.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Kisha, Yawe akanijibu hivi: Uyaandike maono haya; uyaandike wazi juu ya vibao, anayepitia pale apate kuyasoma haraka.


Kisha Yawe akawaambia: Musikilize maneno yangu, kama kuna nabii kati yenu, mimi Yawe ninajifahamisha kwake katika maono na kuongea naye katika ndoto.


Na yote yaliyoandikwa zamani katika Maandiko Matakatifu yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi, kusudi tuendelee kuchunga tumaini kwa njia ya kuvumilia na kufarijiwa sawa tunavyofundishwa katika Maandiko Matakatifu.


Basi nitaendelea kujivuna ijapokuwa si vizuri. Lakini nitasema sasa juu ya maono na ufunuo nilivyopata toka kwa Bwana.


Basi uandike mambo unayoona, na mambo yanayokuwa sasa na yale yatakayotokea nyuma.


Na ngurumo zile saba zilipokwisha kusikilika, nikajitayarisha kwa kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikiniambia hivi: “Uchunge kwa siri maneno yaliyosemwa na zile ngurumo saba.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan