Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 5:7
28 Iomraidhean Croise  

Kulipokuwa asubui, yeye akiwa na wasiwasi sana, aliwaita wachawi wote wa Misri, na wenye hekima, akawaambia ndoto zake. Lakini hakuna hata mumoja aliyeweza kumutafsiria ndoto zile.


Nyuma ya mambo hayo, mufalme Ahasuero akamupandisha Hamani cheo, akakuwa waziri mukubwa. Hamani alikuwa mwana wa Hamedata wa uzao wa Agagi.


Lakini, mufalme wa Misri akawaita wenye hekima wake na wachawi. Wale wachawi wa Misri wakafanya vile vile kwa uchawi wao.


hayo yatakupamba kilemba cha neema juu ya kichwa chako, kama mukufu katika shingo yako.


Pete za masikio zinapendeza mashavu yako. Mikufu ya mawe ya bei kali inapendeza shingo yako.


Wewe umejichokesha bure na washauri wako. Basi, wajitokeze hao wenye akili wakuokoe! Wao wanagawanya mbingu sehemusehemu, wanachunguza nyota na kutabiri kila mwezi yatakayokupata.


Upanga ukuwe juu ya Wakaldea, juu ya wakaaji wa Babeli na wakubwa na wenye hekima wake! –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nikakupamba kwa mapambo, nikakuvalisha vikomo kwa mikono yako na mukufu kwenye shingo.


Jambo lolote la hekima au la maarifa ambalo mufalme aliwauliza alijionea mwenyewe kwamba vijana wale wane walikuwa bora mara kumi kuliko waaguzi na wachawi wote katika utawala wake.


Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.


Basi, mufalme akaamuru waganga, walozi na wachawi wa Wakaldea waletwe kusudi wamufasirie ndoto yake. Wote wakakuja na kusimama mbele yake.


Danieli akamujibu mufalme: Hakuna wenye hekima, wachawi, waganga wala waaguzi wanaoweza kukujulisha fumbo hilo lako.


Kisha mufalme Nebukadneza akamupandishia Danieli heshima kubwa, akamupa zawadi nyingi kubwakubwa, na kumufanya kuwa mutawala wa jimbo lote la Babeli, na mukubwa wa wenye hekima wote wa Babeli.


Lakini mukiniambia hiyo ndoto na maana yake, nitawapa zawadi, mapato na heshima kubwa. Basi, munijulishe ndoto hiyo na maana yake!


Hii ni hukumu iliyotangazwa na walinzi; ni uamuzi wa wanaokuwa watakatifu, kusudi wanadamu wote kila pahali wapate kutambua kwamba Mungu Mukubwa ana mamlaka juu ya falme zote za wanadamu; yeye anamupatia ufalme mutu yeyote anayemupenda, anamufanya kuwa mufalme hata mutu muzaifu wa mwisho.


Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga,


Wenye hekima na wachawi walipoletwa hapa kusoma na kunielezea maana ya maandiko haya, walishindwa.


Lakini, nimesikia kwamba wewe unaweza kueleza vitendawili na kutambua mafumbo. Basi, kama ukiweza kusoma maandiko haya na kunielezea maana yake, utavalishwa nguo nzuri ya rangi nyekundu na kuvalishwa mukufu wa zahabu katika shingo lako. Utapewa nafasi ya tatu katika ufalme huu.


Pale pale, mufalme Belsasari akaamuru kwamba Danieli avalishwe nguo nzuri nyekundu na mukufu wa zahabu katika shingo. Ikatangazwa kwamba Danieli atakamata sasa nafasi ya tatu katika ufalme.


Nitakupatia heshima kubwa, na chochote utakachoniomba nitakutimizia. Kuja uwalaani watu hawa.


Basi, wazee wa Moabu na Midiani wakapeleka zawadi za uaguzi, wakaondoka kwenda kwa Balamu. Walifika, wakamupa Balamu ujumbe wa Balaki.


Sasa! Kwenda zako. Nilikuwa nimekuahidi kukupa zawadi nyingi, lakini Yawe hakukujalia kupata zawadi hizo, amekunyima!


Waliambiana: “Mumemwona yule mutu aliyejitokeza? Yeye amejitokeza kwa kuwazarau Waisraeli. Mufalme Saulo atamupa mutu yeyote atakayemwua mutu yule utajiri mwingi. Zaidi ya yote, atamupatia vilevile binti yake kusudi amwoe. Tena, watu wa jamaa ya baba yake watakuwa huru, hawatalipa kodi.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan