Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Basi, vile vyombo vya zahabu na feza vilivyokamatwa katika hekalu kule Yerusalema vikaletwa. Mufalme, wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake wakavitumia kwa kunywea.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 5:3
11 Iomraidhean Croise  

Alitwaa vyombo vyote vya nyumba ya Mungu vikubwa na vidogo na hazina ya nyumba ya Yawe na ya mufalme na wakubwa wake. Alivipeleka vyote mpaka Babeli.


Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa, imepanua kinywa chake mpaka mwisho. Waheshimiwa pamoja na watu wengine wa Yerusalema wanaingia humo makundi kwa makundi, vilevile na wote wanaushangilia kwa furaha.


Sikiliza! Wakimbizi na wenye kutoroka kutoka inchi ya Babeli wanakuja kutangaza huko Sayuni jinsi Yawe, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.


Kutokana na kunywa divai, mufalme Belsasari akatoa amri kwamba vile vyombo vya zahabu na feza ambavyo baba yake mufalme Nebukadneza alivyokamata kutoka hekalu la Yerusalema, viletwe kusudi avitumie kwa kunywea divai pamoja na wakubwa wake, wanawake wake na wahabara wake.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Walikunywa na kusifu sanamu za miungu iliyotengenezwa na zahabu, feza, shaba, chuma, miti na mawe.


Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.


Kisha wanasonga mbele kama upepo, wanapita na kufanya makosa. Nguvu zao ndio mungu wao!


Lakini ninyi munalizarau jina langu pale munapoichafua mazabahu yangu, na chakula munachotoa juu yake munakizarau.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Wakati ule hakukukuwa bado mufalme katika Israeli. Kulikuwa Mulawi mumoja aliyeishi kama mugeni mbali katika eneo la milima ya Efuraimu. Mutu yule alitwaa habara kutoka Betelehemu katika inchi ya Yuda.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan