Basi, mufalme Nebukadneza akaukaribia mulango wa furu la moto mukali, akaita: Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watumishi wa Mungu Mukubwa, mutoke mukuje hapa! Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakatoka ndani ya moto.
Kwa sababu hiyo, ee mufalme, sikiliza shauri langu. Achana na zambi zako na maovu yako, utende haki na kuwaonea huruma walioteswa; labda muda wako wa kufanikiwa utarefushwa!
Na sasa, mimi Nebukadneza ninamusifu na kumutukuza na kumuheshimu Mufalme wa mbinguni. Maana matendo yake yote ni ya haki, naye anawashusha wenye kiburi.
Ninatoa amri katika ufalme wangu kwamba watu wote wanapaswa kumwogopa na kumuheshimu Mungu wa Danieli. Yeye ni Mungu Mwenye Uzima, anayeishi milele; ufalme wake hauwezi kuangamizwa hata kidogo, utawala wake hauna mwisho.
Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.