Danieli 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20027 Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha. Faic an caibideil |
Yule nyama uliyemwona alikuwa yuko zamani, lakini sasa hayuko tena. Naye ni tayari kupanda toka katika shimo la kuzimu na kwenda kuangamizwa kabisa. Nao wakaaji wa dunia ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangia kuumbwa kwa dunia, watashangaa wakati watakapomwona yule nyama, kwa sababu alikuwa yuko zamani lakini hayuko sasa, naye atatokea tena!
Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.