Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Na yeyote ambaye hatainama chini na kuiabudu, atatupwa mara moja katika furu la moto mukali.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 3:6
20 Iomraidhean Croise  

Akiwa pale, akatazama chini pande za Sodoma na Gomora na eneo lote la bonde, akashangaa kuona moshi ukipanda, moshi kama wa furu kubwa.


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


Sehemu iliyobaki ya muti huohuo, anajichongea nayo mungu, anajifanyia sanamu yake, kisha anapiga magoti mbele yake na kuiabudu. Wanaomba mbele yake wakisema: Wewe ni mungu wangu, uniokoe!


Kwa sababu jambo hilo litakalowapata, watu wote waliohamishiwa Babeli kutoka Yuda, watatumia mufano huu kwa kutoa laana: Yawe akufanye kama Zedekia na Ahabu, ambao mufalme wa Babeli aliwachoma katika moto.


Mufalme akawaambia: Nimetoa neno langu kamili: ikiwa hamutanijulisha ndoto yenyewe na maana yake, mutakatwa vipandevipande na nyumba zenu zitabomolewa.


Na kwamba mutu yeyote asiyeinama chini na kuiabudu sanamu hiyo, atupwe ndani ya furu la moto mukali.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Basi, vijana hao wakafungwa wakiwa wamevaa makoti yao, kanzu zao, kofia na nguo zao zingine, wakatupwa katikati ya ile furu la moto mukali.


Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.


Kwa sababu ya ukubwa aliomupa, watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote walitetemeka na kumwogopa. Nebukadneza aliweza kumwua mutu yeyote aliyetaka na kumwacha muzima mutu yeyote aliyetaka. Aliyetaka kumupandisha cheo alimupandisha, aliyetaka kumushusha cheo alimushusha.


Basi, hao wakubwa na maliwali wote pamoja, wakamwendea mufalme na kumwambia: Uishi milele ee mufalme Dario!


Nao watawatupa ndani ya furu la moto, na mule watalia na kusaga meno.


Na halafu watawatupa watu wabaya ndani ya furu la moto; na mule watalia na kusaga meno.”


Halafu akamwambia: “Nitakupa hivi vyote, kama ukipiga magoti mbele yangu na kuniabudu.”


Mara moja mufalme akamutuma mumoja wa waaskari wake walinzi na kumwamuru aende kuleta kichwa cha Yoane Mubatizaji. Yule askari akaenda ndani ya kifungo na kumukata Yoane kichwa.


Na moshi wa ule moto wa mateso yao utakuwa ukipanda juu kwa milele na milele. Wale walioabudu yule nyama na sanamu yake na mutu yeyote aliyepigwa chapa ya jina lake, hawatapumzika hata siku moja usiku na muchana.”


Nyota ile ikafungua hilo shimo. Moshi unaokuwa kama moshi wa furu kubwa ukapanda toka ndani ya shimo lile. Giza la ule moshi uliotoka ndani ya lile shimo ulifunika jua na anga.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan