Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mutangazaji wa habari akatangaza kwa sauti kubwa: Enyi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote, munaamuriwa kwamba

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 3:4
13 Iomraidhean Croise  

Basi, katika siku ya makumi mbili na tatu ya mwezi wa tatu inayoitwa Siwani, Mordekayi akawaita waandishi wote wa mufalme, akawaagiza waandike barua kwa Wayuda na wakubwa, watawala na wakubwa wa majimbo yote mia moja makumi mbili na saba, kuanzia Uhindi mpaka Etiopia. Barua hizo zikaandikwa kwa kila jimbo katika luga yake na sawasawa na maandiko yake, vilevile na kwa Wayuda kwa maandiko yao na luga yao.


Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Wewe, ee mufalme, ulitoa amri kwamba kila mutu anaposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na kila aina ya muziki, ainame chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu.


Basi, maliwali, wasimamizi, watawala, washauri, walinzi wa hazina, wana sheria na wakubwa wote wa majimbo wakakusanyika tayari kwa muzinduo wa sanamu mufalme Nebukadneza aliyosimamisha.


Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.


Mimi, Nebukadneza, nilikuwa ninaishi katika raha na amani katika nyumba yangu ya kifalme.


Hii ni hukumu iliyotangazwa na walinzi; ni uamuzi wa wanaokuwa watakatifu, kusudi wanadamu wote kila pahali wapate kutambua kwamba Mungu Mukubwa ana mamlaka juu ya falme zote za wanadamu; yeye anamupatia ufalme mutu yeyote anayemupenda, anamufanya kuwa mufalme hata mutu muzaifu wa mwisho.


Mufalme akaamuru wale watu waliomuchongea Danieli wakamatwe, nao wakatupwa ndani ya lile pango la simba pamoja na wake wao na watoto wao. Nao, hata mbele hawajagusa chini, simba waliwashambulia na kuivunjavunja mifupa yao.


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu, na mumefuata mashauri yao. Kwa hiyo nitawaletea maangamizi, na kila mutu atawazarau. Watu watawachekelea kila pahali.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan