Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 2:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Lakini mukiniambia hiyo ndoto na maana yake, nitawapa zawadi, mapato na heshima kubwa. Basi, munijulishe ndoto hiyo na maana yake!

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 2:6
8 Iomraidhean Croise  

Kisha mufalme Nebukadneza akamupandishia Danieli heshima kubwa, akamupa zawadi nyingi kubwakubwa, na kumufanya kuwa mutawala wa jimbo lote la Babeli, na mukubwa wa wenye hekima wote wa Babeli.


Pale pale, mufalme Belsasari akaamuru kwamba Danieli avalishwe nguo nzuri nyekundu na mukufu wa zahabu katika shingo. Ikatangazwa kwamba Danieli atakamata sasa nafasi ya tatu katika ufalme.


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


Nitakupatia heshima kubwa, na chochote utakachoniomba nitakutimizia. Kuja uwalaani watu hawa.


Balaki akamwambia Balamu: Kwa nini haukukuja kwangu mara moja nilipokuita? Ulifikiri sitaweza kukupatia heshima ya kutosha?


Basi, wazee wa Moabu na Midiani wakapeleka zawadi za uaguzi, wakaondoka kwenda kwa Balamu. Walifika, wakamupa Balamu ujumbe wa Balaki.


Sasa! Kwenda zako. Nilikuwa nimekuahidi kukupa zawadi nyingi, lakini Yawe hakukujalia kupata zawadi hizo, amekunyima!


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan