Danieli 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
5 Mufalme akawaambia: Nimetoa neno langu kamili: ikiwa hamutanijulisha ndoto yenyewe na maana yake, mutakatwa vipandevipande na nyumba zenu zitabomolewa.
Ninaamuru vilevile kwamba mutu yeyote ambaye hatatii amri hii, muti mumoja uongolewe kutoka katika nyumba yake na atundikwe juu yake. Tena, nyumba yake ifanywe kuwa yalala.
Kwa hiyo, ninaamuru kwamba watu wa kabila lolote, taifa lolote au luga yoyote, watakaosema kitu chochote cha kumuzarau Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watakatwa vipandevipande na nyumba zao zitabomolewa. Maana hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa namna hii.
Majani yake yalikuwa mazuri. Ulikuwa umejaa matunda mengi yaliyotoshelea kwa kulisha dunia nzima. Nyama wote wa pori walipata kivuli chini yake, na ndege wa anga walikaa katika matawi yake. Viumbe vyote vilipata chakula kutoka muti huo.
Wakati ule Yoshua akaapa mbele ya watu akisema: “Atakayeujenga tena muji wa Yeriko, alaaniwe na Mungu. Yeyote atakayeweka musingi wa muji huo, muzaliwa wake wa kwanza akufe. Yeyote atakayejenga mulango wa muji huo, mwana wake kitenda mimba akufe.”
Samweli akasema: “Kwa sababu upanga wako umewafanya wamama wengi wasikuwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mutoto kati ya wamama.” Akamukatakata Agagi vipandevipande mbele ya Yawe kule Gilgali.