Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 2:49 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

49 Danieli akamwomba mufalme, naye mufalme akawaweka Sadiraki, Mesaki na Abedenego kuwa wasimamizi wa mambo ya utawala ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli akabakia katika nyumba ya mufalme.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 2:49
12 Iomraidhean Croise  

Wabinti walipokusanyika mara ya pili, Mordekayi alikuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme.


Wakati Mordekayi alipokuwa anaikaa kwenye mulango wa mufalme, Bigitani na Teresi, wawili kati ya matowashi wa mufalme waliokuwa walinzi wa milango ya vyumba vya mufalme, walikasirika hata wakafanya shauri baya la kumwua mufalme Ahasuero.


Mufalme akaamuru wakubwa wote wa serikali yake wamutii Hamani kwa kuinama na kupiga magoti mbele yake. Lakini Mordekayi hakuinama wala kupiga magoti mbele yake.


Watu wa haki wakipata madaraka, kuna utukufu mukubwa. Lakini waovu wakitawala, watu wanajificha.


(Basi wakubwa hawa wote wa mufalme wa Babeli waliingia na kukaa kwenye mulango wa katikati: Nergali-Sarezeri, Samgari-Nebo, Sarsekimu jemadari mukubwa wa na Nergali-Sarezeri mukubwa wenye maarifa, pamoja na wakubwa wengine wote wa mufalme wa Babeli.)


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.


Kisha, Danieli akarudi kwa nyumba, akawajulisha wenzake Hanania, Misaeli na Azaria jambo hilo.


Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu, yenye urefu wa metre makumi mbili na nane na upana wa metre tatu. Akaisimamisha katika bonde la Dura katika jimbo la Babeli.


Mufalme Dario aliamua kuweka wakubwa mia moja na makumi mbili kwa kusimamia mambo ya ufalme.


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan