Danieli 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Wale Wakaldea wakamwambia mufalme katika luga ya Kiaramu: Uishi milele, ee mufalme! Utuelezee ndoto yako nasi watumishi wako tutakufasiria maana yake.
Wakaita lundo lile “Lundo la ushuhuda”. Labani akaliita katika kiaramea Yegari-Sahaduta; Yakobo akaliita katika kiebrania Galedi. Labani akasema: “Lundo hili ni ushuhuda kati yako na mimi leo.”
Kulipokuwa asubui, yeye akiwa na wasiwasi sana, aliwaita wachawi wote wa Misri, na wenye hekima, akawaambia ndoto zake. Lakini hakuna hata mumoja aliyeweza kumutafsiria ndoto zile.
Kwa maana leo alienda kutoa sadaka ya ngombe, wana-ngombe wanono na kondoo wengi na amewaalika wana wote wa mufalme, Yoabu jemadari wa waaskari, na kuhani Abiatari, na sasa wanakula na kunywa mbele yake, na kusema: ‘Mufalme Adonia aishi!’
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia, Sebuna na Yoa wakamujibu yule jemadari: “Tafazali, useme nasi kwa luga ya Kiaramea maana tunaielewa. Usiseme nasi kwa luga ya Kiebrania. Watu wanaokuwa juu ya ukuta wanasikia.”
Tena wakati wa utawala wa Artasasta, mufalme wa Persia, Bisilamu, Mitiredati, Tabeli na warafiki zao, wakamwandikia barua mufalme Artasasta. Barua hiyo iliandikwa katika herufi za Kiaramea na kutafsiriwa.
Nikamujibu: “Ee mufalme, uishi milele! Kwa nini nisikuwe mwenye huzuni wakati Yerusalema ambamo makaburi ya babu zangu uko tupu na milango yake imeteketezwa kwa moto?”
Kisha Eliakimu, Sebuna na Yoa wakamujibu yule jemadari: “Tafazali useme nasi kwa luga ya Kiaramea maana tunaielewa. Usiseme nasi kwa luga ya Kiebrania. Watu wanaokuwa juu ya ukuta wanasikia.”
Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.
Majani yake yalikuwa mazuri. Ulikuwa umejaa matunda mengi yaliyotoshelea kwa kulisha dunia nzima. Nyama wote wa pori walipata kivuli chini yake, na ndege wa anga walikaa katika matawi yake. Viumbe vyote vilipata chakula kutoka muti huo.
Kutokana na kelele za mufalme na wakubwa wake, mama ya mufalme aliingia ndani ya chumba cha karamu, akasema: Uishi milele, ee mufalme! Si lazima mawazo yako yakufazaishe na rangi yako kubadilika.
Alipofika karibu akamwita Danieli kwa sauti ya huzuni: Danieli, mutumishi wa Mungu Mwenye Uzima, Mungu wako unayemutumikia siku zote ameweza kukuokoa na simba hawa?
Halafu wakapatana hivi: Hatutapata kisingizio chochote cha kumushitaki Danieli isipokuwa kama kisingizio hicho kitakuwa kinaelekea Sheria ya Mungu wake.
Nalo kundi la watu waliomutangulia Yesu na lile la watu waliofuata nyuma yake, wakaanza kulalamika, wakisema: “Usifiwe wewe Mwana wa Daudi! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Mungu asifiwe juu mbinguni!”
Samweli akawaambia watu wote: “Huyu ndiye mutu aliyechaguliwa na Yawe kati ya watu wote; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye.” Watu wote wakapiga kelele: “Mufalme aishi milele.”