Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Basi, mufalme akaamuru waganga, walozi na wachawi wa Wakaldea waletwe kusudi wamufasirie ndoto yake. Wote wakakuja na kusimama mbele yake.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 2:2
16 Iomraidhean Croise  

Kulipokuwa asubui, yeye akiwa na wasiwasi sana, aliwaita wachawi wote wa Misri, na wenye hekima, akawaambia ndoto zake. Lakini hakuna hata mumoja aliyeweza kumutafsiria ndoto zile.


Ilikuwa desturi ya mufalme kupata mashauri kutoka kwa wenye hekima, hivyo akawaita wanasheria na waamuzi kusudi wamushaurie la kufanya.


Lakini, mufalme wa Misri akawaita wenye hekima wake na wachawi. Wale wachawi wa Misri wakafanya vile vile kwa uchawi wao.


Nitawaondolea Wamisri uhodari wao. Nitaivuruga mipango yao. Watatafuta shauri kwa sanamu na mizimu, wachawi, mizuka na pepo.


Watu wamoja watawaambia ninyi: Muombe shauri kwa mizimu na waaguzi wanaolia kama ndege; kwa sababu ni kawaida watu kuomba shauri kwa miungu yao, na kuomba shauri kwa wafu kwa ajili ya wanaokuwa wazima.


Jambo lolote la hekima au la maarifa ambalo mufalme aliwauliza alijionea mwenyewe kwamba vijana wale wane walikuwa bora mara kumi kuliko waaguzi na wachawi wote katika utawala wake.


Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.


Wale Wakaldea wakamujibu: Mufalme, hakuna mutu yeyote katika dunia anayeweza kutimiza mapenzi yako. Hakuna mufalme yeyote, hata akuwe mukubwa na mwenye nguvu yapata gani aliyepata kuwauliza waganga au walozi au Wakaldea jambo kama hilo.


Danieli akamujibu mufalme: Hakuna wenye hekima, wachawi, waganga wala waaguzi wanaoweza kukujulisha fumbo hilo lako.


Wakati huo, watu wamoja kati ya Wakaldea wakajitokeza na kuwashitaki Wayuda. Walimwambia mufalme Nebukadneza:


Hivyo, nikaamuru wenye hekima wote wa Babeli waletwe mbele yangu kusudi wanielezee maana ya ndoto hiyo.


Ee Beltesaza, unayekuwa mukubwa wa waganga, ninafahamu kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba hakuna fumbo linalokuwa gumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu; uniambie maana yake.


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


Wafilistini waliwaita makuhani na waaguzi wao na kuwauliza: “Tufanye nini na Sanduku hili la Yawe? Mutuambie namna gani tunavyoweza kulirudisha kwa nafasi yake.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan