Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kusikia hivyo, mufalme Nebukadneza alikasirika na kuwa na hasira sana, akaamuru wenye hekima wote wa Babeli waangamizwe.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 2:12
14 Iomraidhean Croise  

Kweli mahangaiko yanamwua mupumbafu, na wivu unamwangamiza mujinga.


wakati ulipoinuka kutimiza hukumu, kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.


Hasira ya mufalme ni kama mujumbe wa kifo; mutu mwenye hekima ataituliza.


Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.


Kasirani kali ya mufalme ni kama simba anayenguruma; anayemukasirikisha anahatarisha maisha yake.


Mwenye kasirani anachochea ugomvi, mutu wa hasira anasababisha makosa mengi.


Basi, Danieli akamwendea Arioki aliyekuwa amechaguliwa kuwaangamiza wenye hekima wa Babeli, akamwambia: Usiwaue wenye hekima wa Babeli, lakini unipeleke mimi mbele ya mufalme, nami nitamweleza maana ya ndoto yake.


Mufalme akawaambia: Nimetoa neno langu kamili: ikiwa hamutanijulisha ndoto yenyewe na maana yake, mutakatwa vipandevipande na nyumba zenu zitabomolewa.


Halafu mufalme Nebukadneza, akakasirika, akaamuru Sadiraki, Mesaki na Abedenego waletwe mbele yake. Nao wakawaleta mbele ya mufalme.


Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.


Kwa sababu ya ukubwa aliomupa, watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote walitetemeka na kumwogopa. Nebukadneza aliweza kumwua mutu yeyote aliyetaka na kumwacha muzima mutu yeyote aliyetaka. Aliyetaka kumupandisha cheo alimupandisha, aliyetaka kumushusha cheo alimushusha.


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan