Halafu, mufalme wa kusini, kwa hasira yake, atapigana vita na mufalme wa kaskazini ambaye naye atamushambulia kwa kundi kubwa la waaskari, lakini litashindwa.
Mashua kutoka Kitimu zitamushambulia, naye atashikwa na hofu. Kisha atarudi nyuma akiwa amejaa hasira na kuvunja agano takatifu. Halafu atafuata shauri la wale walioasi agano takatifu.
Zaidi ya hayo, atapiga mahema yake makubwa kati ya bahari na mulima mutukufu na mutakatifu. Lakini atakuwa amefikia ukomo wake, na hakutakuwa mutu yeyote wa kumusaidia.
Malaika wa sita akamwanga kikombe chake katika muto mukubwa Furati. Maji yake yakakauka kusudi njia itengenezwe kwa ajili ya wafalme wanaotoka mashariki.