42 Wakati atakaposhambulia inchi hizo, hata inchi ya Misri haitaponyoka.
Nitawafanikisha tena Wamisri. Nitawarudisha katika inchi ya Patro, inchi yao ya asili. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu,
Atashambulia hata inchi ile tukufu na kuua maelfu ya watu. Lakini inchi za Edomu, Moabu na sehemu kubwa ya Amoni, zitaokoka kutoka katika mikono yake.
Atatwaa akiba za zahabu, feza na mawe yote ya bei kali ya inchi ya Misri. Watu wa Libya na watu wa Etiopia watamufuata.
Ikiwa kuna taifa lolote katika dunia ambalo halitakwenda Yerusalema kumwabudu Yawe wa majeshi anayekuwa mufalme, basi, mvua haitanyesha katika inchi yao.
Maiti zao zitabaki katika barabara ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa fumbo Sodoma au Misri. Ni ndani ya muji ule Bwana wao alitundikwa juu ya musalaba.