Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 11:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Atawashawishi kwa werevu wale walioasi agano, lakini watu wanaokuwa waaminifu kwa Mungu wao watasimama imara na kutenda.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 11:32
27 Iomraidhean Croise  

“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”


Yawe ni kikingio cha watu wanaoonewa; yeye ni kikingio katika nyakati za taabu.


Mushuhuda mwongo hatakosa kuazibiwa; anayesema uongo hataepuka azabu.


Anayesema uongo anachukia wale anaowaumiza, naye anayebembeleza analeta maangamizi.


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Mufalme atakayefuata atakuwa wa kuzarauliwa ambaye asiyeweza kupewa heshima ya kifalme, naye atakuja wakati watu wasiouzania na kunyanganya ufalme kwa werevu.


Wakati wanapouawa, watapata musaada kidogo, na wengi wanaojiunga nao, watafanya hivyo kwa unafiki.


Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Kila mumoja wao akapewa kanzu nyeupe, wakaambiwa wapumzike kwa muda kidogo mpaka wakati hesabu ya watumishi wenzao na wandugu watakaouawa vilevile kama wao itakapotimia.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan