Danieli 11:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
14 Wakati huo watu wengi watamwasi mufalme wa kusini. Watu wamoja waovu wa taifa lako wewe Danieli, wataasi kwa kutimiza maono haya, lakini watashindwa.
Maana kwa mwisho mufalme wa kaskazini atatayarisha kundi kubwa la waaskari kuliko lile la mbele. Kisha miaka michache atarudi na kundi kubwa la waaskari lenye vifaa vingi vya vita.
Halafu mufalme wa kaskazini atalundika udongo kando ya muji wenye kuta imara na kuuteka. Waaskari wa kusini hawataweza kuupiganisha, hata wale wafundi wa vita, maana hawatakuwa na nguvu.
Kwa maana Mungu ametia ndani yao nia ya kuwasukuma kutimiza shabaha yake nao wapate kufikia shauri moja na kumupa yule nyama madaraka yao ya kifalme mpaka maneno ya Mungu yatimie.