Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 11:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Maana kwa mwisho mufalme wa kaskazini atatayarisha kundi kubwa la waaskari kuliko lile la mbele. Kisha miaka michache atarudi na kundi kubwa la waaskari lenye vifaa vingi vya vita.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 11:13
6 Iomraidhean Croise  

Kisha kulishinda vibaya kundi la waasakri wa kaskazini na kuua maelfu, ataanza kujisifu, lakini hataendelea kuwa mushindi.


Wakati huo watu wengi watamwasi mufalme wa kusini. Watu wamoja waovu wa taifa lako wewe Danieli, wataasi kwa kutimiza maono haya, lakini watashindwa.


Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.


Yule mutu aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani, akainua mikono yake yote miwili kuelekea mbinguni. Kisha nikamusikia akiapa kwa jina la yule anayeishi milele: Itakuwa muda wa nyakati tatu na nusu. Wakati mateso ya watu watakatifu yatakapokomeshwa, mambo haya yote yatakuwa yametimia.


Basi, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, akashangaa kwa muda, na mafikiri yake yakamufazaisha. Mufalme akamwambia: Beltesaza, ndoto hii, wala maana yake visikufazaishe! Beltesaza akamujibu: Bwana wangu, ingelikuwa heri ndoto hii na maana yake iwaelekee waadui zako!


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan