Kwa hiyo yeye akaniambia: Danieli, usiogope. Mungu alisikia maombi yako tangu siku ile ya kwanza ulipoamua kujinyenyekeza mbele yake kusudi upate ufahamu. Mimi nimekuja kwa ajili ya maombi yako hayo.
Atabeba sanamu za miungu yao na vyombo vya bei kali vya feza na zahabu mpaka katika inchi ya Misri. Kwa muda wa miaka michache, mufalme wa kusini hatamushambulia mufalme wa kaskazini.
Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mulango wa lile pango. Mufalme akapiga muhuri wake mwenyewe na ule wa wakubwa wake, kusudi uamuzi uliotolewa juu ya Danieli usibadilishwe.
Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.