Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 10:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 10:1
28 Iomraidhean Croise  

Ndoto yako ilirudiliwa mara mbili kwa mifano inayofanana kwa kukuonyesha kwamba Mungu ameamua, naye atatimiza jambo hili sasa hivi.


Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Kiro mufalme wa Persia, kusudi litimie neno la Yawe alilolisema kwa njia ya nabii Yeremia, Yawe aliamusha nia ya Kiro naye akatoa amri hii katika ufalme wake wote, vilevile alituma habari hizo kwa njia ya maandiko:


Watu walitoa feza za kuwalipa waseremala na wajengaji, walitoa vilevile chakula, vinywaji na mafuta, kusudi vipelekwe katika miji ya Tiro na Sidona kubadilishwa na miti ya mierezi kutoka Lebanoni. Miti hiyo ililetwa kwa njia ya bahari mpaka Yopa. Haya yote yalifanyika kwa musaada wa mufalme Kiro wa Persia.


Lakini Zerubabeli, Yesua na viongozi wengine wa ukoo za Waisraeli wakawaambia: “Sisi hatuhitaji musaada wowote kutoka kwenu kwa kuijenga nyumba ya Mungu wetu. Sisi wenyewe tutamujengea Yawe, Mungu wa Israeli, kama vile mufalme Kiro wa Persia alivyotuamuru.”


Tena wakawalipa wakubwa wa serikali ya Persia kituliro kusudi wapinge kazi ya Wayuda. Wakaendelea kufanya hivyo muda wote wa utawala wa Kiro, mpaka wakati wa utawala wa Dario.


Viongozi wa Wayuda waliendelea vizuri sana na kazi ya ujenzi wa hekalu, wakitiwa moyo na nabii Hagai na Zakaria mwana wa Ido. Wakamaliza ujenzi wa hekalu kama walivyoamriwa na Mungu wa Israeli, na kama walivyoagizwa na mufalme Kiro, mufalme Dario na mufalme Artasasta, wa Persia.


“Katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mufalme Kiro alitoa amri kwamba nyumba ya Mungu ijengwe upya katika Yerusalema, na ikuwe pahali pa kutolea sadaka na sadaka za kuteketezwa kwa moto. Urefu wake kwenda juu utakuwa metre makumi mbili na saba na upana wake metre makumi mbili na saba.


Ndimi ninasema juu ya mufalme Kiro: Ni muchungaji niliyemuchagua kwa ajili yangu. Yeye atatimiza mipango yangu yote. Ndimi ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema utajengwa tena upya; na juu ya hekalu: Musingi wako utawekwa tena.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Danieli alidumu katika kazi ya nyumba ya mufalme mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa mufalme Kiro.


Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.


nami nimekuja kukusaidia upate kuyafahamu mambo yatakayowapata watu wako wakati unaokuja, maana maono uliyoona yanaelekea wakati unaokuja.


Sasa nitakuelezea ule ukweli wa mambo haya. Wafalme wengine watatu wataitawala inchi ya Persia. Hao watafuatwa na mufalme wa ine ambaye atakuwa tajiri kuliko wale waliomutangulia. Wakati atakapopata nguvu kwa ajili ya utajiri wake, ataanza kuushambulia ufalme wa Ugriki.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Akanijibu: Danieli, ujiendee, maana maneno haya ni siri na yamefungwa kwa kutiwa muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho.


Anabadilisha nyakati na wakati, anaondoa na kuwatawalisha wafalme. Anawapa hekima wenye hekima, anawaongezea wenye maarifa ufahamu.


Muti uliendelea kukomaa, ukakuwa imara na kilele chake kikafika mbinguni. Uliweza kuonekana kutoka kila pahali katika dunia.


kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kufasiria ndoto, kufumbua mafumbo na kutatua matatizo. Jina la mutu huyo ni Danieli ambaye baba yako alimwita Beltesaza. Basi wamwite, naye atakuelezea maana ya maandiko haya.


Danieli akamujibu mufalme Belsasari: Unaweza kubakia na zawadi zako, ee mufalme, au kumupa mutu mwingine. Hata hivyo, ee mufalme, nitakusomea maandiko hayo na kukuelezea maana yake.


Yeye anakomboa na kuokoa, anafanya miujiza na maajabu mbinguni na katika dunia, maana amemwokoa Danieli toka nguvu za simba.


Nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka katika muto Ulayi ikiita: Gabrieli, umwelezee mutu huyu maana ya maono aliyoona.


Maono ya hizo nyakati za magaribi na za asubui ambayo yameelezwa ni ya kweli. Lakini uyafiche, sababu ni siri, maana yatatokea kisha siku nyingi.


Maneno yale yatatimia kwa wakati wake uliopangwa, lakini kwa sababu haukuyasadiki, utakuwa bubu. Hautaweza kusema mpaka siku ile mambo hayo yatakapotimia.”


Halafu malaika akaniambia: “Andika maneno haya: Heri wale wanaoalikwa kwa karamu ya ndoa ya Mwana-Kondoo.” Naye akasema tena: “Maneno haya ni ya kweli yanayotoka kwa Mungu.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan