Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini Danieli aliamua kutojichafua kwa kula chakula bora cha mufalme na kunywa divai yake. Kwa hiyo, alimwomba yule mukubwa amuruhusu asikule vitu hivyo na kujichafua.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 1:8
22 Iomraidhean Croise  

Siku zote za utawala wake, watu wa Yuda na wa Israeli walikaa salama, kila mutu akistawi kwenye miti yake ya mizabibu na ya tini.


Kisha wakajiunga kumwabudu Bali kule Peori, wakakula sadaka zilizotambikiwa kwa mizimu.


Nimeapa na kuhakikisha kiapo changu, kwamba nitashika maamuzi yako ya haki.


Muondoke kwangu, enyi waovu, kusudi nipate kushika amri za Mungu wangu.


Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishugulishe na matendo maovu, nisijiunge na watu wanaotenda mabaya, wala nisishiriki hata kidogo katika karamu zao.


Usitamani vyakula vyake vizuri, maana vinaweza kukudanganya.


Mufalme aliagiza vijana wale wapewe chakula bora ambacho yeye mwenyewe alikula na divai ambayo alikunywa. Aliagiza vilevile vijana wale wafundishwe kwa miaka mitatu, kisha wapelekwe kwa mufalme.


Walikunywa na kusifu sanamu za miungu iliyotengenezwa na zahabu, feza, shaba, chuma, miti na mawe.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Lakini inafaa tuwaandikie kwa kuwaambia kwamba wajitenge na vitu vilivyochafuliwa kwa kutambikia sanamu, waepuke uasherati na wasikule nyamafu wala damu.


Lakini inawezekana kwa mutu yule kuchunga kusudi lake bila kushurutishwa. Akiweza kutimiza sawa na mapenzi yake, akiamua kwamba hataki kumwoa muchumba wake, basi yeye anafanya vizuri kutomwoa.


Basi inafaa kila mutu atoe sawa alivyokusudia, si kwa huzuni wala si kwa kulazimishwa. Kwa maana Mungu anapenda mutu yule anayetoa kwa furaha.


Iko wapi hiyo miungu iliyokula matoleo yenu na kunywa divai na sadaka zenu za kinywaji? Basi isimame, iwasaidie; muache hiyo ikuwe ulinzi wenu sasa!


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan