Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 1:7
13 Iomraidhean Croise  

Mufalme akamupa Yosefu jina la Kimisri: Safenati-Panea. Akamupa Asenati, binti ya Potifera, kuhani wa muji wa Oni kuwa muke wake. Basi, Yosefu akaanza kutembelea inchi nzima ya Misri.


Neko mufalme wa Misri akamuweka Eliakimu mwana wa mufalme Yosia kwa pahali pa baba yake Yosia, akabadilisha jina lake kuwa Yoyakimu. Lakini alimupeleka Yoahazi mbali. Naye akafika Misri na kukufia kule.


Nebukadneza akamuweka Matania, baba mudogo ya Yoyakini, kuwa mufalme kwa pahali pake, akalibadilisha jina lake kuwa Zedekia.


Mufalme alipozungumuza nao wote, hakuna walioonekana kuwa bora kama Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria. Basi, wakakubaliwa kumutumikia mufalme.


Mufalme Nebukadneza akamwamuru Aspenazi, mukubwa wa watumishi wake, amuchagulie kati ya vijana wa Waisraeli wa jamaa ya kifalme na ya watu wenye heshima.


Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Kiro wa Persia, Danieli, aliyeitwa vilevile Beltesaza, alipewa ufunuo. Ufunuo huo ulikuwa wa kweli, lakini ulikuwa mugumu sana. Hata hivyo alielewa ufunuo huo maana alifahamu maono vilevile.


Mufalme akamwuliza Danieli, ambaye vilevile aliitwa Beltesaza: Unaweza kunijulisha ndoto niliyoota na maana yake?


Danieli akamwomba mufalme, naye mufalme akawaweka Sadiraki, Mesaki na Abedenego kuwa wasimamizi wa mambo ya utawala ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli akabakia katika nyumba ya mufalme.


Kisha, Danieli akafika, anayeitwa vilevile Beltesaza, jina la mungu wangu, ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake, nami nikamwelezea ndoto yangu, nikasema:


Muti uliendelea kukomaa, ukakuwa imara na kilele chake kikafika mbinguni. Uliweza kuonekana kutoka kila pahali katika dunia.


kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kufasiria ndoto, kufumbua mafumbo na kutatua matatizo. Jina la mutu huyo ni Danieli ambaye baba yako alimwita Beltesaza. Basi wamwite, naye atakuelezea maana ya maandiko haya.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan