Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mufalme aliagiza vijana wale wapewe chakula bora ambacho yeye mwenyewe alikula na divai ambayo alikunywa. Aliagiza vilevile vijana wale wafundishwe kwa miaka mitatu, kisha wapelekwe kwa mufalme.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 1:5
14 Iomraidhean Croise  

Yosefu alikuwa na umri wa miaka makumi tatu alipoanza kumutumikia mufalme. Alitoka katika nyumba ya mufalme na kuitembelea inchi yote ya Misri.


Heri kwa wake zako! Heri kwa hawa watumishi wako ambao wanakutumikia siku zote na kusikiliza hekima yako!


Alipatiwa na mufalme posho yake siku kwa siku, kwa muda wa maisha yake yote kufuatana na mahitaji yake.


Heri kwa wake zako! Heri kwa hawa watumishi wako ambao wanasimama siku zote mbele yako na kusikiliza hekima yako!


Usitamani vyakula vyake vizuri, maana vinaweza kukudanganya.


Basi, Yawe akasema hivi: Kama ukinirudilia, nitakurudisha katika hali yako ya mbele, nawe utanitumikia tena. Kama ukisema maneno ya maana, yasiyokuwa ya upuuzi, basi utakuwa musemaji wangu. Watu watakufikia wewe, wala si wewe utakayehitaji kuwaendea.


Mufalme alipozungumuza nao wote, hakuna walioonekana kuwa bora kama Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria. Basi, wakakubaliwa kumutumikia mufalme.


Lakini Danieli aliamua kutojichafua kwa kula chakula bora cha mufalme na kunywa divai yake. Kwa hiyo, alimwomba yule mukubwa amuruhusu asikule vitu hivyo na kujichafua.


Utupe chakula chetu cha kila siku.


Malaika akamujibu: “Mimi ni Gabrieli, anayebaki karibu na Mungu! Nimetumwa kusema nawe, kwa kukuletea habari hii njema.


Utupe chakula chetu cha kila siku.


Basi mukeshe na kuomba kila wakati, kusudi mupate nguvu ya kuepuka mambo hayo yote yatakayotokea, nanyi mupate kuweza kusimama mbele ya Mwana wa Mutu.”


Halafu Saulo alituma ujumbe kwa Yese na kusema: “Umwache Daudi akae hapa anitumikie kwa sababu amepata kukubaliwa mbele yangu.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan