Danieli 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Mufalme Nebukadneza akamwamuru Aspenazi, mukubwa wa watumishi wake, amuchagulie kati ya vijana wa Waisraeli wa jamaa ya kifalme na ya watu wenye heshima.
Alimupeleka Yoyakini mpaka Babeli pamoja na mama ya mufalme, wake za mufalme, wakubwa wa waaskari wake, na wakubwa wa inchi wote. Hao aliwatoa Yerusalema. Akawapeleka katika uhamisho kule Babeli.
Siku zinakuja ambapo vyote vinavyokuwa katika nyumba yako na vitu vyote babu zako walivyokusanya mpaka leo, vitapelekwa Babeli. Hakuna kitu chochote kitakachobaki. –Ni Yawe anayesema hivyo.–
Katika mwezi wa saba, Isimaeli mwana wa Netania, mujukuu wa Elisama, wa ukoo wa kifalme, mumoja wa wasimamizi wa mufalme alifika Misipa kwa Gedalia pamoja na watu kumi. Wakati walipokuwa wakikula chakula kule Misipa,