Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 1:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Mufalme alipozungumuza nao wote, hakuna walioonekana kuwa bora kama Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria. Basi, wakakubaliwa kumutumikia mufalme.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 1:19
11 Iomraidhean Croise  

Yosefu alikuwa na umri wa miaka makumi tatu alipoanza kumutumikia mufalme. Alitoka katika nyumba ya mufalme na kuitembelea inchi yote ya Misri.


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Kuna mutu mwenye akili na maarifa ndani ya kazi? Yule atawatumikia wafalme; hatawatumikia watu wasiofaa.


Basi, Yawe akasema hivi: Kama ukinirudilia, nitakurudisha katika hali yako ya mbele, nawe utanitumikia tena. Kama ukisema maneno ya maana, yasiyokuwa ya upuuzi, basi utakuwa musemaji wangu. Watu watakufikia wewe, wala si wewe utakayehitaji kuwaendea.


Muda ulipotimia ambapo wale vijana wangepelekwa kwa mufalme kama alivyokuwa ameagiza, yule mukubwa akawapeleka vijana wote mbele ya Nebukadneza.


Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.


Mufalme aliagiza vijana wale wapewe chakula bora ambacho yeye mwenyewe alikula na divai ambayo alikunywa. Aliagiza vilevile vijana wale wafundishwe kwa miaka mitatu, kisha wapelekwe kwa mufalme.


Kati ya vijana waliochaguliwa kulikuwa Danieli, Hanania, Misaeli na Azaria, wote wa kabila la Yuda.


Yule mukubwa wa watumishi akawapa majina mengine; akamwita Danieli kwa jina la Beltesaza, Hanania kwa jina la Sadiraki, Misaeli kwa jina la Mesaki na Azaria kwa jina la Abedenego.


Basi, tangazo likaenea kuwa wenye hekima wote wauawe; Danieli na wenzake, nao vilevile wakatafutwa kusudi wauawe.


Kwa hiyo, ninaamuru kwamba watu wa kabila lolote, taifa lolote au luga yoyote, watakaosema kitu chochote cha kumuzarau Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego, watakatwa vipandevipande na nyumba zao zitabomolewa. Maana hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa namna hii.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan