Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Danieli 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda, mufalme Nebukadneza wa Babeli alikwenda Yerusalema, akauzunguka muji.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Danieli 1:1
14 Iomraidhean Croise  

Yoyakimu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na tano alipoanza kutawala, na akatawala akiwa Yerusalema kwa muda wa miaka kumi na mumoja. Jina la mama yake lilikuwa Zebuda binti wa Pedaya wa muji wa Ruma.


Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.


Tena wamoja kati ya watoto wako wanaume watapelekwa, nao watakuwa matowashi watakaotumika katika nyumba ya mufalme wa Babeli.


Katika mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Yoyakimu mwana wa Yosia, juu ya inchi ya Yuda, Yawe alimupa Yeremia ujumbe juu ya watu wa Yuda. Mwaka huo ulikuwa wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mufalme wa Babeli.


Yawe akamutolea Yeremia ujumbe huu wakati wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda:


Lakini Nebukadneza, mufalme wa Babeli alipofika, kuishambulia inchi hii, tuliamua kuja Yerusalema kwa kuepuka waaskari wa Wakaldea na wa Wasuria. Kwa hiyo sasa tunaishi katika muji Yerusalema.


Katika mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Yoyakimu wa Yuda mwana wa Yosia, ujumbe huu wa Yawe ukatolewa kwa Yeremia:


Haya ndiyo maneno nabii Yeremia aliyosema katika mwaka wa ine wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda na Baruku mwana wa Neria akayaandika katika kitabu:


Yawe akatoa ujumbe huu kwa njia ya nabii Yeremia juu ya inchi ya Babeli, ile inchi ya Wakaldea:


Katika siku ya kumi ya mwezi wa tano, mwaka wa kumi na kenda wa utawala wa Nebukadneza, mufalme wa Babeli, Nebuzaradani mukubwa wa waaskari wa mufalme ambaye alimutumikia mufalme wa Babeli, aliingia Yerusalema.


Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliowapeleka katika uhamisho kwa mwaka wa saba wa utawala wake: Wayuda elfu tatu na makumi mbili na watatu.


Basi, Danieli akaletwa mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: Wewe ndiwe Danieli, mumoja wa wafungwa ambao baba yangu mufalme, aliowaleta kutoka inchi ya Yuda?


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan