Yoyakimu alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na tano alipoanza kutawala, na akatawala akiwa Yerusalema kwa muda wa miaka kumi na mumoja. Jina la mama yake lilikuwa Zebuda binti wa Pedaya wa muji wa Ruma.
Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.
Katika mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Yoyakimu mwana wa Yosia, juu ya inchi ya Yuda, Yawe alimupa Yeremia ujumbe juu ya watu wa Yuda. Mwaka huo ulikuwa wa kwanza wa utawala wa Nebukadneza mufalme wa Babeli.
Lakini Nebukadneza, mufalme wa Babeli alipofika, kuishambulia inchi hii, tuliamua kuja Yerusalema kwa kuepuka waaskari wa Wakaldea na wa Wasuria. Kwa hiyo sasa tunaishi katika muji Yerusalema.
Haya ndiyo maneno nabii Yeremia aliyosema katika mwaka wa ine wa utawala wa Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda na Baruku mwana wa Neria akayaandika katika kitabu:
Katika siku ya kumi ya mwezi wa tano, mwaka wa kumi na kenda wa utawala wa Nebukadneza, mufalme wa Babeli, Nebuzaradani mukubwa wa waaskari wa mufalme ambaye alimutumikia mufalme wa Babeli, aliingia Yerusalema.
Basi, Danieli akaletwa mbele ya mufalme, naye mufalme akamwuliza: Wewe ndiwe Danieli, mumoja wa wafungwa ambao baba yangu mufalme, aliowaleta kutoka inchi ya Yuda?