Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




2 Samweli 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Natani akamwambia mufalme: “Kwenda ufanye chochote unachokifikiri ndani ya moyo wako, kwa maana Yawe yuko pamoja nawe.”

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




2 Samweli 7:3
14 Iomraidhean Croise  

Lakini usiku uleule neno la Yawe lilimufikia Natani kusema hivi:


Lakini kuhani Zadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Natani na Simei, na Rei pamoja na walinzi wa Daudi, hawakumwunga Adonia mukono.


Alipofika kwenye mulima kwa mutu wa Mungu, akamushika miguu, naye Gehazi akakaribia kusudi amwondoe. Lakini mutu wa Mungu akamwambia: “Umwache, maana ana uchungu mukali, naye Yawe hakunijulisha jambo hilo.”


Daudi akamwambia Solomono: “Mwana wangu, nilikusudia ndani ya moyo wangu kumujengea Yawe, Mungu wangu, nyumba kwa kumutukuza.


Halafu mufalme Daudi akasimama na kusema: “Enyi wandugu zangu na watu wangu, munisikilize. Nilikusudia ndani ya moyo wangu kujenga nyumba kwa ajili ya Sanduku la Agano la Yawe, kiti cha kuwekea miguu ya Mungu wetu; na nilifanya matayarisho ya kujenga.


Habari za mufalme Daudi toka mwanzo mpaka mwisho juu ya mambo ya utawala wake, uwezo wake, na mambo yaliyomupata yeye, Waisraeli, na falme zote katika inchi zimeandikwa katika vitabu vya nabii Samweli, katika vitabu vya nabii Natani, vilevile katika vitabu vya nabii Gadi.


Mufalme Hezekia alifuata maagizo ambayo Yawe alikuwa amemupa mufalme Daudi kwa njia ya Gadi, nabii wa mufalme na nabii Natani. Hivyo basi, akaweka Walawi katika nyumba ya Yawe, wamoja wao wakiwa na matoazi, wengine vinanda na wengine vinubi. Hiyo ilikuwa amri ya Yawe kwa njia ya manabii wake.


Akumbuke sadaka zako zote; akubali sadaka zako za kuteketezwa.


Uitafute furaha yako kwa Yawe, naye atakujalia unayotamani katika moyo.


Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Yule kijana aliyemubebea silaha akamwambia: “Fanya chochote unachotaka kufanya, mimi niko pamoja nawe maana wazo lako ndilo wazo langu.”


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan