Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zefania 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Hukumu ya Yerusalema

1 Ole wake Yerusalema, muji wa uasi, muchafu, na wenye kujaa watesaji.

2 Hausikilizi onyo lolote, wala haukubali kutii. Haukumutegemea Yawe hata kidogo, wala kumukaribia Mungu wake.

3 Wakubwa wake ni simba wanaonguruma, waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi wasioacha chochote mpaka asubui.

4 Manabii wake ni watu wasiojali na wadanganyifu. Makuhani wake wamevichafua vitu vitakatifu na kuivunja sheria kwa nguvu.

5 Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki, yeye hatendi jambo lolote baya. Kila siku asubui anatangaza hukumu yake, kila kunapopambazuka anaitimiza. Lakini waovu hawana haya hata kidogo.

6 Yawe anasema: Nimeyateketeza kabisa mataifa; kuta zao za kujikinga ni mabomoko. Barabara zao nimeziharibu, na hakuna anayepita ndani yake. Miji yao imekuwa mitupu, bila watu, na bila wakaaji.

7 Nilisema: Hakika katika muji huu watanitii na kukubali kuonywa; hawataacha kukumbuka mara hizo zote nilizowaazibu. Lakini watu wake walizidisha tamaa zao za kufanya matendo yao kuwa upotovu.

8 Kwa hiyo muningojee mimi Yawe, ngoja siku nitakaposimama kutoa mashitaki. Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme, kuyamwangia kasirani yangu, na ukali wa hasira yangu. Dunia yote itateketezwa kwa moto wa kasirani yangu.

9 Wakati huo nitabadilisha luga ya watu, nitawawezesha kusema luga safi kusudi waniite mimi Yawe, na kuniabudu kwa moyo mumoja.

10 Kutoka ngambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika, wataniletea sadaka yangu.

11 Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.

12 Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.

13 Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.


Wimbo wa furaha

14 Imba kwa sauti, ewe Sayuni, piga vigelegele, ee Israeli. Furahi na kushangilia kwa moyo wote, ewe Yerusalema!

15 Yawe amekuondolea hukumu iliyokuwa juu yako, amewafukuza waadui zako. Yawe, mufalme wa Israeli yuko pamoja nawe. Hautaogopa tena hasara.

16 Siku hiyo, Yerusalema utaambiwa: Usiogope, ee Sayuni, usilegee mikono.

17 Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,

18 kama vile katika siku ya sikukuu. Yawe anasema: Nitakuondolea hasara zako, nawe hautahitaji kupata haya kwa ajili yake.

19 Wakati huo, nitawaazibu wote wanaokugandamiza. Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa na kubadilisha haya yao kuwa sifa na utukufu katika dunia yote.

20 Wakati huo nitawakusanya, na kuwafanya mujulikane na kusifiwa kati ya watu wote katika dunia, na kuwarudishia hali yenu njema, nanyi mutaona kwa macho yenu wenyewe. –Ni Yawe anayesema hivyo.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan