Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

ZAKARIA 3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maono ya ine: Kuhani Mukubwa Yoshua

1 Katika maono mengine, Yawe alinionyesha Kuhani Mukubwa Yoshua akisimama mbele ya malaika wa Yawe, na kwa upande wake wa kuume Shetani alisimama kwa kumushitaki.

2 Malaika wa Yawe akamwambia yule Shetani: Yawe akulaani, ewe Shetani! Kweli, Yawe aliyechagua Yerusalema akulaani! Huyu ni kama kipande cha kuni kilichoopolewa ndani ya moto!

3 Kuhani Mukubwa Yoshua alikuwa akisimama mbele ya malaika, akiwa amevaa nguo zenye kuchafuka.

4 Malaika akawaambia watumishi wake: Muvue Kuhani Mukubwa Yoshua nguo zake zenye kuchafuka. Kisha akamwambia Kuhani Mukubwa Yoshua: Nimeiondoa zambi yako, nami nitakupatia nguo za bei kali.

5 Kisha akawaambia wamuvalishe kitambaa safi juu ya kichwa. Hivyo, wakamuvalisha kitambaa safi na nguo; naye malaika wa Yawe alikuwa akisimama pale.

6 Malaika wa Yawe akamwonya Kuhani Mukubwa Yoshua, akamwambia:

7 Yawe wa majeshi anasema hivi: Ukifuata njia zangu na kushika maagizo niliyokupa, basi, utaisimamia nyumba yangu na viwanja vyake. Nami nitakuwezesha kuingia katika utumishi wangu kama hawa wanaosimama mbele yangu.

8 Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.

9 Mukumbuke kwamba nimeweka mbele ya Yoshua jiwe moja lenye nyuso saba. Nami nitachora maandiko juu yake, na kwa siku moja tu, nitaiondoa zambi ya inchi hii. Kweli, ni mimi Yawe wa majeshi ninayesema hivyo.

10 Siku hiyo, kila mumoja wenu atamwalika mwenzake kufurahia amani na utulivu katika shamba lake la mizabibu na la tini.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan