ZAKARIA 1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu anawaita watu wake wamurudilie 1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido kusema hivi: 2 Yawe alichukizwa sana na babu zenu. 3 Basi, uwaambie watu kwamba: Yawe wa majeshi anasema hivi: Munirudilie nami nitawarudilia ninyi. –Ni Yawe wa majeshi anayesema. 4 Musikuwe kama babu zenu. Manabii waliwaambia: Yawe anasema hivi: muachane na mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya. Lakini wao hawakunisikiliza wala hawakunitii. –Ni ujumbe wa Yawe.– 5 Babu zenu, wako wapi? Na manabii, wanaishi milele? 6 Babu zenu hawakupata azabu kwa sababu ya kukataa maagizo yangu na amri nilizowapa kwa njia ya watumishi wangu manabii? Wakati huo, wao waligeuka na kusema kwamba: Yawe wa majeshi alikusudia kututendea kulingana na mienendo yetu na matendo yetu, na kweli ndivyo alivyotutendea. Maono ya kwanza: Farasi 7 Katika siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kumi na moja, ni kusema mwezi wa Sebati, mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la Yawe lilimufikia nabii Zakaria mwana wa Berekia, mujukuu wa Ido. Zakaria akasema hivi: 8 Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe. 9 Basi, nikamwuliza: Bwana, farasi hawa wana maana gani? Malaika yule aliyesema nami akaniambia: Nitakuonyesha wale farasi wana maana gani. 10 Hawa ndio waliotumwa na Yawe kuichunguza dunia. 11 Hao farasi wakamwambia huyo malaika wa Yawe aliyekuwa akisimama katikati ya miti ya mihadasi: Tumeichunguza dunia yote, nayo kweli imetulia. 12 Halafu yule malaika wa Yawe akasema: Ee Yawe wa majeshi, kwa muda gani utaendelea kutokuwa na huruma juu ya muji Yerusalema na miji ya inchi ya Yuda ambayo umeikasirikia kwa muda wa miaka makumi saba? 13 Yawe akamupa yule malaika jibu jema na lenye matumaini. 14 Basi, huyo malaika akaniambia: Tangaza kwa sauti na kusema hivi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Ninasikia wivu sana juu ya Yerusalema na Sayuni. 15 Lakini nimekasirikia sana mataifa ambayo yanastarehe. Nilikuwa ninayakasirikia kidogo, lakini yaliwaongezea hasara. 16 Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema. 17 Kisha malaika yule akaniambia nitangaze ujumbe huu mwingine: Yawe wa majeshi anasema hivi: Miji yake itafurika tena na fanaka. Yawe atafariji tena Sayuni, atachagua Yerusalema kuwa wake. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo