Zaburi 99 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu ni mutawala mukubwa 1 Yawe anatawala, mataifa yanatetemeka! Ameikaa juu ya makerubi, nayo dunia inatikisika! 2 Yawe ni mukubwa katika Sayuni; ametukuzwa kuliko mataifa yote. 3 Wote wasifu jina lake kubwa la kutisha. Yeye ni mutakatifu! 4 Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki. 5 Mumusifu Yawe, Mungu wetu; muiname uso mpaka chini mbele yake. Yeye ni mutakatifu! 6 Musa na Haruni walikuwa makuhani wake; Samweli alikuwa kati ya waliomulilia. Walimulilia Yawe naye akawasikiliza. 7 Alisema nao katika nguzo ya wingu; walitimiza maagizo yake na masharti aliyowapa. 8 Ee Yawe, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza; ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliwaazibu kwa makosa yao. 9 Mumusifu Yawe, Mungu wetu; muiname kwa mulima wake mutakatifu! Yawe, Mungu wetu, ni mutakatifu. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo