Zaburi 96 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu mufalme na mwamuzi ( 1 Sik 16.23-33 ) 1 Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Mumwimbie Yawe, ninyi ulimwengu wote! 2 Mumwimbie Yawe na kusifu jina lake. Mutangaze kila siku matendo yake ya wokovu. 3 Muyatangazie mataifa utukufu wake, muwaambie watu wote matendo yake ya ajabu. 4 Maana Yawe ni mukubwa, anasifiwa sana; anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote. 5 Miungu ya mataifa si kitu; lakini Yawe ndiye aliyeumba mbingu. 6 Heshima na sifa vinamuzunguka; nguvu na uzuri vinajaza hekalu lake. 7 Mumupe Yawe heshima, enyi watu wa kila namna; mutangaze utukufu na nguvu yake. 8 Mumupe Yawe utukufu wa jina lake. Mulete sadaka na kuingia katika viwanja vya hekalu lake. 9 Mumwabudu Yawe katika pahali pake patakatifu; tetemeka mbele yake, ee dunia nzima! 10 Muyaambie mataifa: “Yawe anatawala! Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika. Atahukumu mataifa kama vile inavyofaa.” 11 Mufurahi, enyi mbingu na dunia! Bahari ivume pamoja na vyote vinavyokuwa ndani yake! 12 Mufurahi, enyi mbuga na vyote vinavyokuwa ndani yenu! Halafu miti yote ya pori itaimba kwa furaha, 13 mbele ya Yawe kwa sababu anakuja. Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki, na mataifa kwa uaminifu wake. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo