Zaburi 95 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Wimbo wa kumusifu Mungu 1 Mukuje tumwimbie Yawe, tumushangilie yeye kikingio na mwokozi wetu! 2 Tuende mbele yake na nyimbo za shukrani; tumushangilie kwa nyimbo za sifa. 3 Maana Yawe ni Mungu mukubwa; yeye ni mufalme mukubwa juu ya miungu yote. 4 Mabonde ni katika mikono yake, vilele vya milima ni vyake. 5 Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya; kwa mikono yake aliumba inchi kavu. 6 Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu! 7 Maana yeye ni Mungu wetu. Sisi ni watu wake, kondoo wanaochungwa katika malisho yake. Heri leo mungesikiliza hivi anavyosema: 8 “Musikuwe wagumu kama kule Meriba, kama ilivyokuwa kule Masa katika jangwa, 9 babu zenu waliponijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea. 10 Kwa miaka makumi ine nilichukizwa nao, nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka! Hawajali kabisa njia zangu!’ 11 Basi, nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia kwenye mapumziko niliyowatayarishia.” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo