Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 91 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu mulinzi wetu

1 Ukikaa chini ya ulinzi wa Mungu Mukubwa, ukiishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,

2 utaweza kumwambia Yawe: “Wewe ni kimbilio langu ninamojificha, Mungu wangu ninayemutumainia!”

3 Hakika Mungu atakuokoa katika mutego, atakukinga na magonjwa mabaya.

4 Atakufunika kwa mabawa yake; utapata usalama kwake. Uaminifu wake ni ngao ya kukinga.

5 Hautaogopa vitisho vya usiku, wala shambulio la rafla muchana.

6 Hautaogopa ugonjwa mukali unaotokea usiku, wala hasara inayotokea muchana.

7 Kama watu elfu wakianguka pembeni yako, hata elfu kumi karibu yako, hasara haitakupata.

8 Kwa macho yako mwenyewe utaangalia, na kuona jinsi watu waovu wanavyoazibiwa.

9 Wewe umemufanya Yawe kuwa kimbilio lako; Mungu anayekuwa juu kuwa tegemeo lako.

10 Kwa hiyo, hautapatwa na hasara yoyote; nyumba yako haitakaribiwa na pigo lolote.

11 Maana Mungu atawaamuru wamalaika wake, wakulinde popote unapoenda.

12 Watakuchukua katika mikono yao, kusudi usijikwae kwenye jiwe.

13 Utakanyaga simba na nyoka wa hatari, utawaponda simba wakali na nyoka.

14 Mungu anasema: “Nitamwokoa yule anayenipenda; nitamulinda anayejua jina langu!

15 Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.

16 Nitamupa maisha marefu, nitamujalia wokovu wangu.”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan