Zaburi 87 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Sifa ya Yerusalema 1 Zaburi ya Wakora: Wimbo. Mungu amejenga muji wake juu ya mulima wake mutakatifu. 2 Yawe anapenda Sayuni, kuliko makao mengine ya Yakobo. 3 Ee muji wa Mungu, mambo ya utukufu yanasemwa juu yako. 4 Kati ya wale wanaonijua mimi, kuna Wamisri na Wababeli. Vilevile Wafilistini, Watiro na Waetiopia. Wanasema: “Huyu amezaliwa kule.” 5 Lakini juu ya Sayuni itasemwa: “Sayuni ni mama yao wote; Mungu Mukubwa atauimarisha.” 6 Yawe atakapohesabu watu, ataandika hivi katika kitabu: “Huyu amezaliwa kule!” 7 Wote wanacheza ngoma na kuimba: “Sayuni shina letu ni kwako.” |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo