Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 86 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuomba musaada

1 Maombi ya Daudi. Unitegee sikio, ee Yawe, unijibu, maana mimi ni masikini na mukosefu.

2 Ulinde maisha yangu maana mimi ni mwaminifu mbele yako; uniokoe mimi mutumishi wako ninayekutegemea.

3 Wewe ni Mungu wangu; basi, unionee huruma, maana ninakulilia muchana kutwa.

4 Ee Bwana wetu, ninakutolea moyo wangu. Ufurahishe roho yangu mimi mutumishi wako.

5 Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.

6 Ee Yawe, utegee maombi yangu sikio; usikilize kilio cha ombi langu.

7 Siku za taabu ninakuita, maana wewe unaniitikia.

8 Ee Bwana, hakuna mungu mwingine anayekuwa kama wewe; hakuna anayeweza kufanya unayofanya wewe.

9 Mataifa yote uliyoumba, yatakuja kukuabudu, ee Bwana; yatatangaza ukubwa wa jina lako.

10 Wewe ndiwe mukubwa, unafanya maajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.

11 Unifundishe njia yako, ee Yawe, nipate kuwa mwaminifu kwako; uongoze moyo wangu nikuheshimu.

12 Ee Bwana, Mungu wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitatangaza ukubwa wa jina lako milele.

13 Wema wako kwangu ni mwingi sana! Umeniokoa kutoka katika kuzimu.

14 Ee Mungu, watu wenye kiburi wamenishambulia; kundi la watu wakali lilitaka kuniua, wala halikujali wewe hata kidogo.

15 Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.

16 Unigeukie, unihurumie; unijalie nguvu yako mimi mutumishi wako, umwokoe mutoto wa mujakazi wako.

17 Unionyeshe kitambulisho cha wema wako, ee Yawe, kusudi wale wanaonichukia wafezeheke, wanapoona umenisaidia na kunifariji.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan