Zaburi 85 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuombea taifa baraka 1 Kwa mukubwa wa waimbaji: Zaburi ya Wakora. 2 Ee Yawe, umependelea inchi yako; umerudishia wazao wa Yakobo hali nzuri. 3 Umewasamehe watu wako kosa lao; umefuta zambi zao zote. 4 Umezuia kasirani yako yote; umeacha hasira yako kali. 5 Utustareheshe tena, ee Mungu mwokozi wetu; uondoe chuki unayokuwa nayo juu yetu. 6 Utatukasirikia hata milele? Utadumisha kasirani yako kwa vizazi vyote? 7 Hautatujalia tena maisha mapya, kusudi watu wako wafurahi kwa sababu yako? 8 Utuonyeshe wema wako, ee Yawe, utujalie wokovu wako. 9 Ninasikiliza yale Yawe anayosema, maana anaahidi kuwapa watu wake amani, watu wake mwenyewe wasiporudilia upumbafu wao. 10 Hakika yeye ni tayari kuwaokoa wanaomuheshimu, na utukufu wake utadumu katika inchi yetu. 11 Wema na uaminifu vitakutana; haki na amani vitashikamana. 12 Uaminifu utachipuka katika inchi; haki utashuka toka mbinguni. 13 Kweli, Yawe atatuletea baraka, na inchi yetu itatoa mazao yake mengi. 14 Haki itamutangulia Mungu na kumutayarishia njia yake. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo