Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 83 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maombi juu ya waadui za Israeli

1 Zaburi ya Asafu. Wimbo.

2 Ee Mungu, usikae kimya! Usinyamaze, ee Mungu, wala usitulie!

3 Angalia! Waadui zako wanafanya fujo; wanaokuchukia wanainua vichwa kwa kiburi.

4 Wanafanya mipango mibaya kwa kuwazuru watu wako; wanashauriana juu ya hao unaowalinda.

5 Wanasema: “Mukuje tuangamize taifa lao, hata jina la Israeli lisikumbukwe tena.”

6 Kweli, wanakubaliana kwa moyo moja, wanafanya mapatano juu yako:

7 Waedomu na Waisimaeli, Wamoabu na Wahagari;

8 Wagebali, Waamoni na Waamaleki, Wafilistini na wakaaji wa Tiro.

9 Hata Waasuria wameshirikiana nao, wamewaunga mukono wazao wa Loti!

10 Uwatendee ulivyowatendea Wamidiani, ulivyowatendea Sisera na Mufalme Asikie kwenye muto Kisoni,

11 watu uliowaangamiza kule Endori, wakakuwa takataka juu ya inchi.

12 Uwatendee wakubwa na watawala wao kama Kibombobombo na Mbwa wa Pori, kama Sadaka na Kivuli,

13 ambao walisema: “Tutajitwalia inchi ya Mungu.”

14 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi; kama makapi yanayopeperushwa na upepo.

15 Kama vile moto unavyoteketeza pori, na ndimi za moto zinavyounguza milima,

16 uwakimbize hao kwa zoruba yako, na kuwatisha kwa upepo wako mukali!

17 Ujaze nyuso zao haya, wapate kukutafuta, ee Yawe.

18 Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.

19 Wajue kwamba wewe peke yako, ambaye jina lako ni Yawe, ndiwe Mungu Mukubwa juu ya dunia yote.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan