Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 82 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu ni mutawala mukubwa

1 Zaburi ya Asafu. Mungu anasimamia baraza lake. Anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu:

2 “Mpaka wakati gani mutaendelea kuhukumu bila haki na kuwapendelea watu waovu?

3 Muimarishe sheria yangu kwa wazaifu na wayatima; muwatendee wasiojiweza na wamasikini kwa haki.

4 Muwaokoe wazaifu na wakosefu, muwaopoe kutoka makucha ya waovu.

5 “Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu! Ninyi munatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa!

6 Mimi nilisema kwamba ninyi ni miungu, kwamba ninyi wote ni wana wa Mungu Mukubwa!

7 Hata hivyo, mutakufa kama watu wote; mutaanguka kama mukubwa yeyote.”

8 Simama sasa, ee Mungu, uuhukumu ulimwengu; maana mataifa yote ni mali yako.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan