Zaburi 82 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Mungu ni mutawala mukubwa 1 Zaburi ya Asafu. Mungu anasimamia baraza lake. Anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu: 2 “Mpaka wakati gani mutaendelea kuhukumu bila haki na kuwapendelea watu waovu? 3 Muimarishe sheria yangu kwa wazaifu na wayatima; muwatendee wasiojiweza na wamasikini kwa haki. 4 Muwaokoe wazaifu na wakosefu, muwaopoe kutoka makucha ya waovu. 5 “Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu! Ninyi munatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa! 6 Mimi nilisema kwamba ninyi ni miungu, kwamba ninyi wote ni wana wa Mungu Mukubwa! 7 Hata hivyo, mutakufa kama watu wote; mutaanguka kama mukubwa yeyote.” 8 Simama sasa, ee Mungu, uuhukumu ulimwengu; maana mataifa yote ni mali yako. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo