Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 81 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Wimbo wa sikukuu

1 Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa mutindo wa watu wa Gati. Zaburi ya Asafu.

2 Mumwimbie Mungu kwa sauti, maana ni nguvu yetu, mumushangilie Mungu wa Yakobo,

3 muvumishe wimbo wa shangwe, mupige ngoma, mucheze zeze na kinubi cha sauti nzuri.

4 Mupige baragumu kutangaza mwandamo wa mwezi, na pia mbalamwezi wakati wa sikukuu yetu.

5 Hilo ndilo sharti katika Israeli; hilo ndilo agizo la Mungu wa Yakobo.

6 Aliwapa watu wa Israeli agizo hilo, aliposhambulia inchi ya Misri. Ninasikia sauti nisiyoitambua ikisema:

7 “Mimi nilikutua mizigo yako toka kwenye mabega, nilikuondolea matofali uliyochukua katika mikono.

8 Katika shida uliniita, nami nikakuokoa. Nilikujibu kutokea katika ngurumo. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba.

9 Enyi watu wangu, musikie onyo langu. Heri ungenisikiliza, ee Israeli!

10 Usikuwe na mungu wa kigeni; usiabudu hata kidogo mungu mwingine.

11 Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri. Fungua kinywa chako, nami nitakulisha.

12 “Lakini watu wangu hawakunisikiliza; Israeli hakunitaka kabisa.

13 Hivyo, nikawaacha wabaki katika ugumu; wafuate mashauri yao wenyewe.

14 Heri watu wangu wangenisikiliza! Heri Israeli angefuata njia zangu!

15 Ningewashinda waadui zao haraka; ningenyoosha mukono juu ya wapinzani wao.

16 Wanaonichukia wangenipigia magoti kwa hofu, na azabu yao ingekuwa ya milele.

17 Lakini wewe ningekulisha kwa ngano bora, ningekushibisha kwa asali ya pori.”

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan