Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 75 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Mungu ni mwamuzi wa haki

1 Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu”. Zaburi ya Asafu: wimbo.

2 Tunakushukuru, ee Mungu, tunakushukuru! Tunatangaza ukubwa wa jina lako na kueleza matendo yako makubwa.

3 Mungu anasema: “Mimi nimeweka wakati kamili! Wakati huo nitahukumu kwa haki.

4 Inchi ikitetemeka na vyote vinavyokuwa ndani yake, mimi ndiye ninayeimarisha misingi yake.

5 Ninawaambia wenye kiburi: ‘Mwache kiburi’, na waovu: ‘Musiote mapembe!

6 Musijione kuwa watu wa maana sana, wala kusema maneno ya majivuno.’ ”

7 Ukubwa hautoki mashariki au magaribi, wala hautoki katika jangwa au kwa milima.

8 Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi; anamushusha mumoja na kumwinua mwingine.

9 Yawe anashika kikombe katika mukono, kimejaa divai kali ya hasira yake. Anaimimia, nao waovu wote wanaikunywa; wanaikunywa mpaka tone la mwisho.

10 Lakini mimi nitafurahi milele, nitamwimbia Mungu wa Yakobo sifa.

11 Atavunja mapembe yote ya watu waovu; lakini ataotesha mapembe ya watu wa haki.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan