Zaburi 74 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombolezo 1 Mashairi ya Asafu. Kwa nini, ee Mungu, umetutupilia kabisa? Mbona hasira yako inawaka juu ya kondoo wako? 2 Kumbuka taifa lako ulilojipatia tangia zamani, kabila ulilokomboa likuwe mali yako. Kumbuka mulima Sayuni pahali unapokaa. 3 Pita juu ya mabomoko haya ya tangu zamani! Waadui wameharibu kila kitu katika hekalu. 4 Waadui zako wamepiga kelele la ushindi katika hekalu lako! Wamesimika humo bendera zao za ushindi! 5 Wanafanana na mukataji wa kuni, anayekata miti kwa shoka lake. 6 Walivunjavunja michoro ya hekalu, kwa mashoka na nyundo zao. 7 Waliunguza pahali patakatifu pako; walikufuru pahali pale unapoheshimiwa. 8 Walikusudia kutuangamiza wote pamoja; walichoma pahali pote katika inchi ambapo tulikutana kwa kukuabudu. 9 Hatuoni tena vitambulisho vya kuwa kwako kati yetu, hatuna tena nabii yeyote, wala hakuna anayejua mwisho wa haya yote! 10 Ee Mungu, mpaka wakati gani adui atakuchekelea? Watakufuru jina lako milele? 11 Mbona umeficha mukono wako wa kuume? Kwa nini haunyooshi mukono na kuwapiga? 12 Hata hivyo wewe Mungu ni mufalme wetu tangu zamani; umefanya mambo makubwa ya kuokoa katika inchi. 13 Kwa uwezo wako mukubwa uligawanya bahari; uliponda vichwa vya nyama mukubwa wa bahari. 14 Wewe uliponda vichwa vya nyama mukubwa Leviatani; ukawapa wanyama wa jangwa muzoga wake. 15 Wewe umefanya chemichemi na vijito; na kukausha mito mikubwa. 16 Muchana ni wako na usiku ni wako; umeweka mwezi na jua kwenye nafasi zao. 17 Wewe umeweka mipaka yote ya dunia; umepanga wakati wa kipwa na wakati wa mvua. 18 Kumbuka, ee Yawe, mazarau ya waadui zako; taifa pumbafu linatukana jina lako. 19 Usitutupie, sisi njiwa wako, kwa wanyama wakali, usisahau kwa siku zote maisha ya wamasikini wako. 20 Ukumbuke agano ulilofanya nasi! Inchi imejaa mateso makali kila nafasi za giza. 21 Usiwaache wanaogandamizwa wafezeheshwe, uwajalie wamasikini na wakosefu wasifu jina lako. 22 Ee Mungu, simama sasa ujitetee! Ukumbuke mazarau ya kila siku ya wasiokujua. 23 Usisahau makelele ya waadui zako; na fujo ya siku zote ya wapinzani wako. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo