Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 73 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


SEHEMU YA TATU (Zaburi 73–89 ) Haki itatawala

1 Zaburi ya Asafu. Hakika, Mungu ni muzuri kwa Israeli, kwa watu wenye moyo safi.

2 Nilikuwa karibu sana kujikwaa, kidogo tu ningeteleza,

3 maana niliwaonea wivu wenye kiburi, nilipoona wakosaji wakifanikiwa.

4 Maana hao hawapatwi na mateso; miili yao ina afya, nao wana nguvu.

5 Taabu za mwanadamu haziwapati hao; hawapati mateso kama watu wengine.

6 Kiburi kimekuwa kama mukufu katika shingo, mateso makali ni kama nguo yao.

7 Mazarau yanatokana na unene wao; mioyo yao inatiririka mipango mibaya.

8 Wanawachekelea wengine na kusema mabaya; wanajivuna na kufanya mipango ya utesaji.

9 Kwa vinywa vyao wanatukana mbingu; kwa ndimi zao wanajitapa katika dunia.

10 Hata watu wa Mungu wanawafuata, hawaoni kwao kitu chochote kibaya na kusadiki kila wanachosema.

11 Wanasema: “Mungu hawezi kujua! Mungu Mukubwa hataweza kugundua!”

12 Hivi ndivyo watu waovu wanavyokuwa; wako na kila kitu, nao wanapata hata zaidi.

13 Kweli ni kwa bure nimejichunga katika usafi wa moyo, na kujilinda nisitende zambi?

14 Muchana kutwa ninapata mapigo, kila asubui nimepata mateso.

15 Ningalisema kama wao, ningalikuwa mwenye uasi kati ya watu wako.

16 Basi, nilijaribu kufikiri juu ya jambo hili, lakini lilikuwa gumu sana kwangu,

17 mpaka nilipoingia pahali pako patakatifu. Halafu nikatambua yatakayowapata waovu.

18 Kweli wewe unawaweka pahali penye utelezi; unawafanya waanguke na kuangamia.

19 Wanaangamizwa kwa rafla, wateketezwe kabisa kwa vitisho.

20 Ee Bwana, unapoinuka, wanatoweka kama ndoto, kama ndoto wakati mutu anapoamuka.

21 Nilipoona uchungu katika moyo na kuchomwa katika roho,

22 nilikuwa mupumbafu na mujinga, nilikuwa kama nyama mbele yako.

23 Hata hivyo siku zote niko nawe, ee Mungu! Unanishika mukono wa kuume.

24 Wewe unaniongoza kwa mashauri yako; na kwa mwisho utanipokea kwenye utukufu.

25 Mbinguni, nani anayeweza kunisaidia isipokuwa wewe? Na katika dunia hamuna ninachokitamani isipokuwa wewe!

26 Hata nikikosa nguvu katika mwili na katika roho, wewe, ee Mungu, ni kikingio changu; na hitaji langu lote ni wewe kwa milele.

27 Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.

28 Lakini, kwangu ni vizuri kuwa karibu na Mungu. Wewe Bwana wangu Yawe ndiwe usalama wangu. Nitatangaza mambo yote uliyotenda!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan