Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 72 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kumwombea mufalme

1 Zaburi ya Solomono. Ee Mungu, umujalie mufalme uwezo wa kufuata sheria yako, umupe mwana wa mufalme haki yako.

2 Atawale taifa lako kwa haki, na wamasikini wako kwa sheria yako.

3 Milima ilete ustawi kwa watu wako, vilima vijae haki.

4 Mufalme awatetee wamasikini wa taifa, awasaidie wakosefu, na kuwaangamiza watesaji.

5 Mufalme aishi muda murefu kama jua, na kama mwezi, kwa vizazi vyote.

6 Akuwe kama manyunyu yanayolowanisha mashamba, kama mvua inayonyeshea udongo.

7 Haki istawi maisha yake yote, na amani kwa wingi mpaka mwezi ukome.

8 Atawale kutoka bahari hata bahari, kutoka muto Furati hata miisho ya dunia.

9 Waadui zake wanaokaa katika jangwa wanyenyekee mbele yake, wapinzani wake walambule vumbi.

10 Wafalme wa Tarsisi na visiwa wamulipe kodi, wafalme wa Sheba na Seba wamuletee zawadi.

11 Wafalme wote wa dunia wamuheshimu, watu wa mataifa yote wamutumikie.

12 Atamukomboa mukosefu anayemwomba, na masikini asiyekuwa na wa kumusaidia.

13 Atawahurumia wazaifu na wakosefu, atayaokoa maisha yao wenye shida.

14 Atawatoa katika mateso na ukali, maana maisha yao ni ya bei kubwa kwake.

15 Mufalme aishi maisha marefu; apokee zawadi ya zahabu kutoka Sheba; watu wamwombee kwa Mungu siku zote, na kumutakia baraka muchana kutwa.

16 Inchi itoe mazao kwa wingi, vilima vijae mavuno kama ya Lebanoni, na watu wa miji wastawi kama majani.

17 Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!

18 Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye peke yake anafanya miujiza.

19 Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!

20 Mwisho wa maombi ya Daudi mwana wa Yese.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan