Zaburi 7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Maombi ya mutu anayeteswa 1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Wimbo wa malalamiko ya Daudi, aliomwimbia Yawe kwa ajili ya Kushi wa kabila la Benjamina. 2 Ee Yawe, Mungu wangu, ninakukimbilia wewe. Uniokoe kutoka wote wanaonitesa, uniponyeshe. 3 Kama si vile, watakuja kunirarua kama simba, kunipasua vipandevipande wala hakuna wa kuniokoa. 4 Ee Yawe, Mungu wangu! Kama nimetenda moja ya mambo haya: kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya, 5 kama nimemurudishia rafiki yangu mabaya pahali pa mema, au nimemunyanganya adui yangu bila sababu, 6 basi, adui anifuatilie na kunikamata, akomeshe maisha yangu na kuuzika uzima wangu ndani ya mavumbi. 7 Ee Yawe, kwa hasira yako, simama sasa ukomeshe kasirani ya waadui zangu! Amuka, ee Mungu wangu, wewe umeamuru haki ifanyike. 8 Ukusanye mataifa kandokando yako, nawe uyatawale tokea kule juu. 9 Wewe, ee Yawe, unayehukumu mataifa, unihukumu kadiri ya haki yangu, kulingana na ukamilifu wangu. 10 Ukomeshe uovu wa watu wabaya, uwaimarishe watu wa haki, ee Mungu unayetenda haki, unayejua siri za mioyo na mafikiri ya watu. 11 Mungu ndiye ngao yangu; yeye anawaokoa watu wenye moyo wa usawa. 12 Mungu ni mwamuzi wa haki; kila siku analaumu maovu. 13 Watu wasipogeuka toka ubaya wao, Mungu atanoa upanga wake; atavuta upinde wake na kupima shabaha. 14 Atatayarisha silaha zake za hatari, na kuitia mishale yake moto. 15 Mutu mubaya anatunga uovu, anajaa uharibifu na kuzaa udanganyifu. 16 Anachimba shimo, na kulirefusha, kisha anatumbukia humo yeye mwenyewe. 17 Uharibifu wake utamurudilia yeye mwenyewe; ukali wake utamwangukia yeye mwenyewe. 18 Nitamushukuru Yawe kwa sababu ya haki yake; nitaimba sifa za jina la Yawe, Mungu Mukubwa. |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo