Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 66 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Wimbo wa shukrani

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Wimbo. Zaburi. Enyi wakaaji wote wa dunia, mumushangilie Mungu!

2 Muimbe kwa ajili ya utukufu wa jina lake, mumusifu kwa utukufu!

3 Mumwambie Mungu: “Matendo yako ni ya ajabu! Kwa nguvu yako kubwa waadui zako wanaishiwa nguvu.

4 Dunia yote inakuabudu; watu wote wanakuimbia sifa!”

5 Mukuje muone mambo Mungu aliyotenda; ametenda mambo ya kutisha kati ya watu.

6 Aligeuza bahari kuwa inchi kavu, watu wakapita humo kwa miguu; kwa hiyo nasi tukashangilia.

7 Anatawala milele kwa nguvu yake kubwa; macho yake yanachungulia mataifa yote. Mwasi yeyote asisubutu kumupinga.

8 Mumusifu Mungu wetu, enyi mataifa yote; mutangaze sifa zake zipate kusikilika.

9 Yeye ametujalia maisha, wala hakutuacha tuanguke.

10 Umetupima, ee Mungu, umetujaribu kama madini kwa moto.

11 Umetunasa katika wavu; umetubebesha muzigo muzito.

12 Umewaacha watu watukanyage; tumepitia katika moto na katika maji. Lakini sasa umetuleta kwenye usalama.

13 Nitakuja ndani ya nyumba yako na sadaka za kuteketezwa, nitakutimizia viapo vyangu

14 nilivyotamka na kukuahidia mimi mwenyewe nilipokuwa katika taabu.

15 Nitakutolea sadaka za kuteketezwa za nyama wenye kunona, sadaka za kuteketezwa za kondoo dume; nitatoa sadaka za ngombe dume na beberu.

16 Enyi munaomwabudu Mungu, mukuje wote musikilize, nami nitawaelezea mambo aliyonitendea.

17 Mimi nilimulilia kwa sauti, sifa zake nikazitangaza.

18 Kama ningalikusudia maovu ndani ya moyo, Yawe hangalinisikiliza.

19 Lakini kweli Mungu amenisikiliza; amesikiliza maneno ya maombi yangu.

20 Mungu asifiwe! Hakukataa maombi yangu, wala hakuacha kunitendea mema.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan