Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Maombi wakati wa taabu

1 Kutoka Mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.

2 Ee Yawe, usiniazibu kwa hasira yako, usiniadibishe kwa kasirani yako.

3 Unihurumie, ee Yawe, nimeishiwa nguvu; uniponyeshe, ee Yawe, ninatetemeka mpaka katika mifupa.

4 Ninahangaika sana ndani ya roho yangu. Ee Yawe, utakawia mpaka wakati gani?

5 Unigeukie, ee Yawe, uniokoe; uniponyeshe kwa sababu ya wema wako.

6 Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka; katika kuzimu ni nani anayeweza kukusifu?

7 Ninatabanika kwa kulia kwa uchungu; usiku ninalowanisha kitanda changu kwa machozi; kwa kulia kwangu ninalowanisha matandiko yangu.

8 Macho yangu yamechoka kwa huzuni; yamefifia kwa kutaabishwa na waadui.

9 Muondoke karibu nami, enyi wote watenda maovu! Maana Yawe amesikia kilio changu.

10 Yawe amesikia ombi langu; Yawe amekubali maombi yangu.

11 Waadui zangu wote watafezeheka na kufazaika; watarudi nyuma na kufezeheka kwa rafla.

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan