Zaburi 59 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002Kuomba ulinzi wa Mungu 1 Kiebrania: Kwa mukubwa wa waimbaji: kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu”. Mashairi ya Daudi wakati Saulo alipotuma wapelelezi wamwue. 2 Ee Mungu wangu, uniokoe kutoka waadui zangu, unikinge na hao wanaonishambulia. 3 Uniokoe na hao wanaotenda maovu, Uniponyeshe kutoka hao wauaji! 4 Angalia! Wananivizia waniue. Watu wakali wanachochea ugomvi juu yangu ingawa sikufanya ubaya wowote. 5 Ingawa sina kosa, wanakimbia, ee Yawe, kujiweka tayari. Uinuke, ee Yawe, uwaangalie na kunisaidia! 6 Uinuke, ee Yawe, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli. Uamuke, uwaazibu hao watu wasiokujua; usiwaache hao waasi na wabaya. 7 Kila magaribi waadui hao wanarudi wakifoka kama imbwa, na kuzungukazunguka katika muji. 8 Angalia, ni matusi tu yanayotoka katika midomo yao, maneno yao ni kama panga kali; tena wanafikiri hakuna anayewasikia. 9 Lakini wewe, ee Yawe, unawachekelea; unawazarau hao watu wasiokujua. 10 Nitakungojea, ewe unayekuwa nguvu yangu; maana wewe, ee Mungu, ni kimbilio langu. 11 Mungu wangu mwema sana atakuwa mbele yangu, ataniwezesha kuwaona waadui zangu wameshindwa. 12 Usiwaue mara moja, watu wangu wasisahau; uwasambazesambaze kwa nguvu yako, uwaporomoshe chini. Ee Bwana, wewe ndiwe ngao yetu! 13 Wao wanatenda zambi katika masemi yao yote, kwa hiyo wanaswe katika kiburi chao! Kwa sababu ya laana na uongo wao, 14 uwateketeze kwa hasira yako, uwateketeze watoweke kabisa, kusudi watu wote wajue mpaka kwa miisho ya dunia ya kuwa wewe Mungu unatawala wazao wa Yakobo. 15 Kila magaribi waadui hao wanarudi wakifoka kama imbwa, na kuzungukazunguka katika muji. 16 Wanapitapita huko na huko wakitafuta chakula, nao wasiposhiba wananguruma. 17 Lakini mimi nitaimba sifa za nguvu yako, nitashangilia asubui juu ya wema wako, maana wewe umekuwa kikingio changu, wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. 18 Ewe unayekuwa nguvu yangu, nitakuimbia sifa; ee Mungu, wewe ni kikingio changu, Mungu anayenitendea mema! |
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Bible Society of the Democratic Republic of Congo