Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -

Zaburi 57 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002


Kuomba musaada

1 Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu.” Mashairi ya Daudi alipomuponyoka Saulo na kujificha katika pango.

2 Unihurumie, ee Mungu, unihurumie, maana ninakukimbilia wewe. Ninakimbilia kwenye kivuli cha mabawa yako, mpaka zoruba ya maangamizi ipite.

3 Ninamulilia Mungu Mukubwa, Mungu anayenikamilishia nia yake.

4 Atanipelekea musaada toka mbinguni na kuniokoa, atawafezehesha hao wanaonishambulia. Mungu atanionyesha wema na uaminifu wake!

5 Mimi nimezungukwa na waadui, wenye uchu wa damu kama simba; meno yao ni kama mikuki na mishale, ndimi zao ni kama panga kali.

6 Utukuzwe, ee Mungu, juu katika mbingu! Utukufu wako uenee katika dunia yote!

7 Waadui wamenitegea wavu waninase, nami ninaugua kwa huzuni. Wamenichimbia shimo katika njia yangu, lakini wao wenyewe wametumbukia humo.

8 Moyo wangu ni tayari, ee Mungu, moyo wangu ni tayari; nitaimba na kukushangilia!

9 Amuka, ee nafsi yangu! Muamuke, enyi kinubi na zeze! Nitayaamusha mapambazuko!

10 Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.

11 Wema wako unaenea hata juu katika mbingu, uaminifu wako unafika hata katika mawingu.

12 Utukuzwe, ee Mungu, juu katika mbingu! Utukufu wako uenee katika dunia yote!

Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.

Bible Society of the Democratic Republic of Congo
Lean sinn:



Sanasan